Jumatano , 12th Nov , 2014

Msanii Rema Namakula amefanya sherehe ya ukaribisho wa mtoto maaarufu kama baby shower huko nchini Uganda akikabidhiwa zawadi mbali mbali za uzazi kutoka kwa ndugu na marafiki zake wa karibu.

msanii wa muziki wa Uganda Rema Namakula ambaye ni mjamzito akiwa na mke wa Bobi Wine Barbie

Sherehe hii inua uvumi uliokuwa ukiendelea mtaani kuwa msanii huyu tayari amekwishajifungua mtoto wa kike kwa siri ambapo kujifungua kwake kunatarajiwa wakati wowote kuanzia hivi sasa.

Hadi kufikia katika hatua hii, Rema bado hajataka kuweka wazi baba wa mtoto wake, huku dalili zote zikiendelea kuonyesha kuwa msanii Eddy Kenzo ndiye mhusika wa ujauzito wa staa huyu.