Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nyumba ya Fid Q yanusurika kubomolewa

Jumamosi , 17th Feb , 2018

Mwenyekiti wa serikali za mtaa wa Mbweni Teta, Abdallah Mrisho amefunguka na kudai sio kweli nyumba ya msanii Fid Q imejengwa katika kiwanja kisicho rasmi kwa shughuli za makazi bali watu wanafananisha na eneo hilo na nyumba ya serikali za mtaa huo.

Mrisho ametoa ufafanuzi huo wakati alipokuwa anazungumza na eNewz kutoka EATV baada ya kuibuka tetesi kuwa Fid Q ameingizwa 'mkenge' kwa kuuziwa kiwanja kisicho rasmi katika shughuli za makazi na kulazimika nyumba hiyo aliyojenga kuvunjwa ili kupisha shughuli za serikali ziweze kufanywa.

"Kwa ufahamisho tu zaidi katika upande wa 'block 4' nyumba ya kwanza kabisa ni ya Fid Q na ya mwisho kabisa katika mtaa huu naishi mimi mwenyewe. Labda niwatoe wasiwasi kwa wale waliokuwa wanasikia kwamba Fid Q amejenga nyumba katika eneo la wazi na nyumba kuwa ipo hatari kuvunjwa niseme tu hapana labda hawakuweza kupambanua kati ya nyumba yake na nyumba ya ofisi za serikali za mtaa kwa sababu hivi vitu vinashabiana", amesema Mrisho.

Kwa upande wake, Fid Q alipofuatwa kuzungumzia suala hilo hakuweza kusema lolote zaidi ya kusema anashukuru.

Mtazame hapa chini Fid Q akishikwa na kigugumizi kuzungumzia suala hilo.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa