Ijumaa , 11th Sep , 2015

Msomi na Msanii wa muziki Noah PV ameongezea nguvu harakati za kampeni kuhamasisha watanzania kushiriki katika zoezi zima la kupiga kura, na hii ni kupitia projekti ambayo inasimama kwa jina 'Kura Yako'.

Msomi na Msanii wa muziki Noah PV

Hii inakuwa ni moja ya kazi bora yenye ujumbe unaowataka watanzania kuwa sehemu ya maamuzi ya mustakabali wa nchi yao kutokana na kutambua umuhimu wa kupiga kura kuelekea katika uchaguzi mkuu mwezi ujao.

Noah PV, ameeleza kuwa rekodi ya ushiriki hafifu wa watanzania katika uchaguzi katika kipindi cha nyuma ndio moja ya sababu kubwa zilizomsukuma kufanya kazi unayoitazama sasa kama anavyoeleza mwenyewe hapa.