Ijumaa , 10th Jun , 2016

Msanii wa Bongo Movie aliyetamba sana na 'kiki' la ugomvi kati yake na Hemed PHD,Yusufu Mlela amefunguka juu ya dili lake la nchini kenya.

Msanii wa Bongo Fleva Yusufu Mlela

Akizungumza na Enewz Mlela amesema kuwa anashukuru Mungu kwakuwa hiyo ndiyo nafasi kwake katika kuiwakilisha nchi yetu.

“Project yangu ya Kenya imenipa Exposure kubwa sana kiasi kwamba imenitanua katika kila kitu na watu wategemee kitu kikubwa zaidi”, amesema Mlela huku akiongezea kuwa majukumu ya familia ndiyo yalimfanya atulie zaidi na kuwa kimya huku akihusika zaidi na kazi zake pekee.