Alhamisi , 12th Feb , 2015

Msanii ma muziki wa Injili, Emmanuel Mbasha amesema kuwa pembeni ya changamoto anazopitia katika maisha yake binafsi, anamshukuru Mungu kwa kuweza kukamilisha albam yake ya muziki yenye nyimbo 10 ambayo imeweza kupokelewa vizuri sana mitaani.

Msanii wa muziki wa injili nchini Tanzania Emmanuel Mbasha

Emmanuel amesema kuwa, rekodi ambazo zipo katika albam hiyo zinabeba ujumbe wa kutia moyo ikiwa ni msukumo alioupata kutoka katika matatizo ambayo amekuwa akipitia, na hapa anaeleza mwenyewe juu ya kazi hiyo.