Jumamosi , 3rd Oct , 2015

Star wa muziki Mabeste, ameweka wazi siri kubwa iliyokuwa nyuma ya ngoma yake ya Sirudi Tena iliyomtambulisha vizuri katika game, kuwa aliandika kutokana na hisia za machungu alizokuwa nazo baada ya kukosana na timu aliyokuwa akifanya nayo kazi BHitz

Mabeste

Mabeste amesema kuwa, kazi hiyo ilifanyika baadaye chini ya studio hiyo hiyo baada ya kumsikilizisha producer Pancho Latino ambaye licha ya mistari ya rekodi yenyewe kuwa ilikuwa ikimdiss, aliielewa na kusuka mdundo wake na baadaye kufanyika kuwa moja ya rekodi kubwa kabisa za Mabeste.

Mabeste hivi sasa pia amerejea kwa kishindo katika game, ambapo usiku wa jana ametambulisha video mpya ya rekodi yake ya Usiwe Bubu katika show kali ya FNL.

Haya ni maneno ya Mabeste kuhusiana na Diss ya Sirudi Tena ambayo iligeuka kuwa ngoma bora ya kuhamasisha maendeleo kutoka kwake.

Tags: