Jumanne , 18th Feb , 2025

Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva Estelina Sanga maarufu kama Linah amefunguka kuwa wimbo wake wa Oletemba wenye jumla ya miaka kumi umemletea mafanikio makubwa kwenye muziki wake.

Pichani Linah Sanga

Akizungumza na mwandishi wetu Linah ameeleza kuwa wimbo huo wa Oletemba umemfanya kukutana na wasanii wakubwa wa nchi tofauti tofauti lakini pia umeweka rekodi ya kuwa msanii wakwanza katika Era yake kufanya kazi nje ya nchi.

 

 Linah pia ameeleza kuwa kwa kipindi kile kilichomkwamisha kuendelea kukimbizana na spidi ya kimataifa ni uongozi uliyokuwa unamsimamia msanii huyo, mbali na hayo pia ameweka wazi kuwa mipango mikubwa ambayo anayo kwasasa ni kuhakikisha anarudi kwenye muziki na huenda akaja na album.