
Msanii wa muziki wa nchini Uganda Iryn Namubiru
Sherehe ya kutunikiwa shahada kwa msanii huyu inafanyika leo nchini Uganda katika Chuo Kikuu cha Cavendish wakati ambapo msanii huyu yupo huko Uingereza kwa shughuli zake za kimuziki.
Hatua hii ambayo amepiga Iryn imeelezwa na wadau kuwa mfano wa kuigwa kwa mabinti nchini Uganda na Afrika Mashariki kwa ujumla kutokana na umuhimu wa swala zima la Elimu katika dunia ya sasa.