Jumamosi , 7th Feb , 2015

Star mkongwe katika game ya muziki hapa Bongo, Dudu Baya ambaye amekuwa kimya kisanaa kwa muda sasa, amesema kuwa hiyo inatokana na kutokuwa katika muziki kwa muda mrefu.

Dudu Baya

Amesema hakuwa katika muziki kwa muda mrefu akiwa anachukua muda wake sasa kufanya mambo mengine kabla ya ujio wake mpya kwa mwaka 2015.

Dudu Baya amesema kuwa, yeye sio aina ya msanii ambaye hutangaza michakato yake kabla ya haijakamilika, na kwa mashabiki ambao wanamsikilizia star huyu neno lake kwao ni kuwa atafanya vitu na vitatokea kwa mwaka huu.