Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Dkt. Mwakyembe aitumbua Miss Tanzania

Jumatatu , 25th Sep , 2017

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe amesema wizara yake imefuta mashindano ya Miss Tanzania kwa sababu yaligubikwa na ubabaishaji mwingi katika uendeshaji wake.

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe.

Dkt. Mwakyembe ameeleza hayo baada ya kupita takribani miezi mitatu tokea alipokabidhiwa zawadi yake Miss Tanzania 2016/2017, Diana Edward ambayo ilizua maneno mengi katika mitandao ya kijamii wakidai zawadi hiyo ya gari waliyompatia Miss huyo ilikuwa imechakaa na kupewa nje ya wakati na kushusha hadhi ya mashindano hayo pamoja na kuvunja moyo kwa watu ambao walikuwa na lengo la kushiriki katika mashindano mengine yajayo.

"Mimi na wizara yangu tuna mikakati tofauti kabisa, tungependa vitu vyote tunavyo vianzisha viwe na muendelezo na siyo vianzishwe leo keshokutwa vimekatika. Niwatolee mfano kidogo tulikuwa na Miss Tanzania hapa chini lakini nimepiga marufuku kwa sababu ya uswahili mwingi ambao mimi siwezi kuukubali nikiwa kiongozi wa hii wizara, kwa hiyo nimewakatalia wote hakuna cha miss Tanzania", amesema Dkt. Mwakyembe.

Pamoja na hayo, Dkt. Mwakyembe ameendelea kwa kusema "Endapo watataka kuendesha hayo mashindano nitahitaji zawadi ya mshindi wa kwanza kama ni gari iletwe ofisini kwangu niione na waniachie funguo yake pia zawadi ya mshindi wa pili hivyo hivyo ndipo nikaporuhusu. Maana kila mwaka zawadi ya mshindi wa kwanza imekuwa ikisumbua kutolewa kwa muhusika. Sasa huo mchezo hapana, hatuwezi kuona ukiendelea, ubabaishaji siyo kwa Tanzania ya leo"

Kwa upande mwingine, Dkt. Mwakyembe amesema sasa anachokifanya ni kukaa chini na baadhi ya wadau wa masuala ya 'fashion' ili waweze kuyaboresha mashindano hayo yaweze kuwa bora na kufanyika kila mwaka bila ya kuwa na ubabaishaji.

HABARI ZAIDI

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani