Jumanne , 11th Mei , 2021

Msanii wa Nigeria Davido anatuhumiwa kwa wizi wa wimbo ‘Jowo’ kutoka kwa mwimbaji Victor AD.

Picha ni Msanii Davido

Mtumiaji wa Twitter aliyejitambulisha kama “Thug Life” alimtuhumu Superstar huyo wa afrobeats kuwa mwaka 2020 aliiba kazi ya Victor AD baada ya Davido kusikia wimbo huo wakiwa studio wanarekodi wimbo wa Victor AD 'Tire You'  na baada ya hapo inadaiwa alimzumzuia (block)  kwenye mitandao yote ya kijamii.

Sio Davido wala Victor AD wametoka kuthibitisha taarifa hizi ambazo zinaendelea kasambaa kupitia mtandao wa Twitter