Ijumaa , 9th Oct , 2015

Nyota wa muziki wa dansi nchini Coco Chanel ambaye imepita miaka nane tokea aondoke FM Academia ametoa ya moyoni kuhusiana na kusepa kwake akisema kuwa ni maamuzi yake tu ya kutafuta maisha nje ya bendi akiendeleza biashara zake.

Coco ambaye alitamba katika video ya wimbo uitwao 'Anna' akiwa na bendi yake hiyo ameiambia Enewz kuwa kuondoka kwake haimaanishi hatoiimbia tena bendi hiyo, kwani ni hivi karibuni tu aliweza kuitwa kupaform na bendi hiyo ilipofanya sherehe ya miaka 18 tokea kuanzishwa kwake.

Coco Chanel afunguka zaidi kupitia enewz kuhusiana na hili.