Alhamisi , 8th Jul , 2021

Ni tambo za mashabiki wa Simba na Yanga baada ya mechi ya Julai 3 na kuelekea fainali ya kombe la FA Julai 25 ambapo msanii mkongwe wa filamu Bibi Mwenda amempa makavu Haji Manara kwa kusema anabwabwaja sana hivyo wanataka kumfundisha adabu.

Msanii mkongwe wa filamu Bibi Mwenda na Msemaji wa Klabu ya Simba Haji Manara

Akizungumza hilo mbele ya Camera za EATV & EA Radio Digital, baada ya Haji Manara kusema wachezaji wa Yanga ni wa kuokota Bibi Mwenda amesema

"Kwanza tumewafunga moja tu ili liliwatie hasira, tulitaka kumfundisha adabu Haji Manara kwa sababu anabwabwaja sana na anazungumza maneno mengi, aingie uwanjani aone ugumu wa mpira sio kuongeaongea" 

"Anasema sisi tunaokota wachezaji kumbe yeye ndio anaokota sasa na kimbembe amekiona juzi, nawahusia wana Yanga wote Tanzania kwamba tumeshawafunga hapa Dar bado kule Kigoma" ameongeza 

Mengine zaidi aliyoyazungumza tazama hapo chini kwenye video.