Alhamisi , 7th Mei , 2015

Msanii wa muziki wa Injili Angel Benard, amezungumzia muelekeo wa muziki wa Injili katika wakati huu wa sasa ambapo kumekuwa na muingiliano mkubwa na muziki wa kawaida, ambao unafanywa na wasanii wengine kwa lengo la kuburudisha.

Msanii wa muziki wa Injili Angel Benard wa nchini Tanzania

Akiwa kama moja ya wasanii wa kizazi kipya waliofanikiwa kwa upande wa Gospel, Angel amesema kuwa, miziki ya dunia na ile ya injili yote ni sawa, ingawa kuna umuhimu wa kuwa na mipaka na kusimamia misingi ya rekodi za injili.

Vilevile msanii huyu akaongea juu ya ujio wa kazi yake mpya, msikilize hapa.