Jumatano , 1st Jul , 2015

Star wa muziki Barnaba, amejinadi kuwa albamu yake mpya itaingia sokoni kwa bei ya dola 100 ama zaidi, pesa ambazo zinakadiriwa kufikia shilingi laki 2 za Tanzania kwa nakala 1.

msanii wa miondoko ya bongofleva nchini Barnaba

Mkali huyo amekuwa akijiamini kutokana na ubora wa nyimbo, utofauti na uwekezaji mkubwa anaoendelea kuufanya kukamilisha kazi hiyo.

Barnaba ameeleza kuwa, baadhi ya rekodi kutoka albam hizo zimekwishapelekwa nchi mbalimbali ikiwepo Afrika Kusini na Ujerumani kwaajili ya 'Mastering', zikitarajiwa kutoka kwa mfumo wa DVD, na vile vile CD za kawaida, kwa bei hiyo ambayo hata hivyo amesisitiza kuwa inaweza kuongezeka zaidi.