Makubi ameyasema hayo leo Julai 4, 2021 jijini Dodoma ambapo amesema wananchi hawatatozwa fedha ili kupata chanjo.
''Muongozo wa kuingiza na kutoa chanjo umekamilika na mtu atachomwa kwa hiari yake na chanjo zitatolewa bure. Serikali haitaruhusu uingizwajI wa chanjo kiholela na kuwatoza wananchi fedha kwaajili ya chanjo'',ameeleza Prof. Abel Makubi.
Prof. Makubi amesema wamechukua hatua hizo ili kuwakinga wananchi na sio kusubiri hadi hali iwe mbaya ndio hatua zichukuliwe.
''Sisi kama serikali hatuwezi kusubiri mpaka watu wananchi wengi waathirike, tuna wajibu wa kulinda afya ya kila mwananchi, hatuwezi kusubiri mpaka idadi iwe kubwa, kwetu serikali mwananchi hata kama ni mmoja ni muhimu kwetu,'' amesema Prof. Abel Makubi.
Soma taarifa kamili hapo chini











