Alhamisi , 1st Mei , 2014

Idadi kubwa ya wanafunzi katika madarasa ya shule za msingi nchini Tanzania umeelezwa kuchangia kwa kiasi kikubwa cha wanafunzi kufeli katika mitihani yao ya kuhitimu elimu ya msingi.

Hayo yameelezwa na walimu wanaofundisha shule za msingi jijini Dar es salaam wakati Tanzania ikiungana na nchi nyingine Duniani katika kuadhimisha siku ya wafanyakazi Duniani.

Wakizungumza na EATV baadhi ya walimu hao wamesema uwiano uliopo kati ya walimu na wanafunzi madarasani hauridhishi ambapo mwalimu mmoja analazimika kufundisha wanafunzi zaidi ya 90 huku uwiano stahiki ni mwalimu mmoja kufundisha wanafunzi 45.