Jumatatu , 11th Oct , 2021

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD) Meja Jenerali Gabriel Saul Mhidze ahakikishe mpaka kufikia Jumamosi, Oktoba 16, 2021 dawa ziwe zimepatikana katika maeneo yote nchini.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa

Waziri Mkuu amesema kuwa ni maelekezo ya Serikali kuwa vituo vyote vya kutolea huduma zikiwamo zahanati, vituo vya afya, hospitali za wilaya, hospitali za rufaa za mikoa lazima zipate dawa kwa kuwa zinategemea MSD.

Tazama video hapo chini