Waziri Jafo akiwa na wanafunzi
Waziri Jafo ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), jijini Dodoma ambapo amesema watoto kupata elimu ni haki yao.
"Ni marufuku kuwazuia watoto kusajiliwa kuanza Darasa la kwanza, ila wale ambao hawana vyeti vya kuzaliwa wazazi na RITA ihakikishe ndni ya miezi mtoto anapata cheti cha kuzaliwa."
#HABARI Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo (Mb) amepiga marufuku watoto kuzuiliwa kuandikishwa darasa la kwanza sababu ya hana cheti cha kuzaliwa. pic.twitter.com/5kDdZs99iD
— East Africa Radio (@earadiofm) January 8, 2020

