Jumamosi , 19th Jul , 2014

Wazee wilayani Butiama mkoa wa Mara, wamelaani vikali kauli zinazotolewa na baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba zinazoashiria kejeli kwa waasisi wa Taifa la Tanzania

Baadhi ya wazee wilayani Butiama katika mkutano wao na mkuu wa wilaya hiyo.

 
Wakati bunge la katiba likitarajia kuanza  vikao vyake  mwezi ujao, wazee  kutoka  koo nane  za  kabila  la wazanaki  katika  wilaya  ya  Butiama mkoani  Mara, wamelaani  vikali  kauli  za  kejeli  na  matusi zinazoelekezwa  kwa  waasisi wa muungano hayati  mwalimu Julius Kambarage Nyerere na hayati  Abeid Aman Karume kwa kile  ambacho  wamekisema ni kukosa  heshima  kwa  mchango  mkubwa  wa waasisi  hao.

Wazee hao  wametoa tamko  hilo wakiwa makao makuu  ya wilaya ya Butiama  mbele  ya  mkuu  wa  wilaya hiyo, ambapo  wamesema kuwa hayati mwalimu Julius Nyerere licha ya kuzaliwa katika kijiji cha Butiama mkoani Mara hakuwa mbinafsi katika utawala wake hivyo  kauli la kejeli na matusi dhidi yake zinazotolewa na baadhi ya wajumbe wa bunge la katiba ni kumkosea  heshima.
 
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Butiama Bi Angelina Mabula, akijibu tamko hilo la wazee wa Butiama amesema  watanzania leo  wanapaswa kutambua wametoka wapi, wapo wapi na  wanakwenda wapi na pia umuhimu wa waasisi hao.