Jumatatu , 19th Oct , 2020

Baba na mama lishe katika kituo cha mabasi Mbagala, Jijini Dar es Salaam, wamesena walipata hasara ya kulazimika kumwaga chakula wakati ambapo barabara ya kuingia kituo cha mabasi Mbagala ilipofungwa hivyo kwa sasa wanaishukuru serikali kwa kusikia kilio chao kwa kuifungua barabara hiyo.

Baba Ntilie wa kituo cha mabasi cha Mbagala

Wakizungumza na Kurasa leo baba na mama lishe hao wamesema idadi kubwa ya wateja wanaowategemea ni abiria hivyo wakati ilipofungwa barabara hiyo mabasi yalikuwa hayaingii  kituoni hapo hali iliyokuwa inawasabishia hasara kutokana na kutopata wateja.

“Kwa sasa tunaishukuru serikali imefungua hii barabara sasa mabsdi yanaingia kwa wakati nmyakiwa na abiria” amesema Mariam mama lishe katika kituo hicho

Kwa upande wake katibu wa kituo hicho, Yusuph Ismail, amesema mapato yameongezeka kwa sasa kutokana na idadi ta mabasi yanayoingia kituoni hapo kuongezeka.