Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watu watokwa damu, Figo zafeli na watano wafariki

Alhamisi , 16th Mar , 2023

Wizara ya Afya imesema inafuatilia ugonjwa usiojulikana uliotokea mkoani Kagera wilaya ya Bukoba vijijini ambapo watu saba walipata dalili za homa, kutapika, kutokwa damu maeneo mbalimbali ya miili yao na Figo kushindwa kufanya kazi, ambapo watano wamefariki dunia na wawili wako hospitali.

Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Tumaini Nagu,

Wizara ya imesema inafuatilia ugonjwa usiojulikana uliotokea mkoani Kagera na kuua watu watano baada ya watu saba kupata dalili za homa, kutapika, kutokwa damu maeneo mbalimbali ya miili yao na Figo kushindwa kufanya kazi, ambapo wawili wako hospitali.

Taarifa hiyo imetolewa leo Machi 16, 2023, na Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Tumaini Nagu, na kusema Ugonjwa huo usiojulikana umetokea wilaya ya Bukoba vijijini katika vijiji vya Bulinda na Butayaibega, ambapo inasadikiwa watu hao saba walipata dalili hizo za homa.

"Serikali imechukua hatua za kudhibiti ugonjwa huo ili usisambae kwa kuchukua sampuli kutoka kwa wagonjwa na waliofariki ili kubaini chanzo cha ugonjwa huo na ufuatiliaji wa watu wenye viashiria vya ugonjwa kwenye jamii," amesema Profesa Nagu.

Aidha Profesa Nagu ameongeza, "Pia dawa, vifaa na vifaa tiba muhimu vipo katika vituo vya kutolea huduma za afya mkoani Kagera na wagonjwa wanaendelea na matibabu, na elimu ya afya inaendelea kutolewa kwa jamii mkoani Kagera ili kuchukua tahadhari,"- Profesa Tumaini Nagu, Mganga Mkuu wa Serikali

Katika hatua nyingine Wizara ya Afya imewatoa hofu Watanzania kuhusu ugonjwa huo na kushauri, "Mtu yeyote mwenye dalili za homa, kutapika, kuharisha, kutoka damu na mwili kuishiwa nguvu anashauriwa kuwa kituo cha kutolea huduma za afya, kuepuka kumgusa mgonjwa au majimaji ya mwili, mate, machozi, damu, mkojo na kinyesi kitokacho kwa mgonjwa au yeyote mwenye dalili hizo,".
 

 

HABARI ZAIDI

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%