Jumanne , 11th Jan , 2022

Watu watano wakiwemo waandishi wa  habari wamefariki katika  ajali ya gari huku wengine wakijeruhiwa katika ajali iliyohusisha magari mawili kugongana uso kwa uso wilayani Busega mkoani Simiyu asubuhi ya leo Januari 11, 2022.

Moja ya gari zilizopata ajali

Gari aina ya Toyota Land Cruiser lililokuwa limebeba waandishi wa habari waliokuwa wanakwenda wilayani Ukerewe kwenye ziara ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza Eng. Evarist Ndikilo, limegongana uso kwa uso na gari ndogo ya abiria (Hiace) na kusababisha vifo hivyo.

Picha ya gari lililopata ajali

Taarifa kutoka Ofisi ya Mkoa wa Mwanza zinaeleza kuwa ziara hiyo imeahirishwa huku wakibainisha kuwa miongoni mwa watu watano waliofariki pia yupo Ofisa habari na mahusiano wa mkoa wa Mwanza Bwana Abel Ngapema.

Watu wakitoa huduma ya kuwatoa majeruhi eneo la ajali

Wengine waliofariki ni wanahabari Husna Mlanzi wa ITV, Vanny Charles wa Icon, Johari Shani wa Uhuru Digital.

Miili ya waliofariki imehifadhiwa katika Kituo cha Afya Nassa wilayani Busega mkoani Simiyu.