Moja ya mwili aliyepigwa risasi
Majambazi hao walifika katika mtaa huo kwa lengo la kuvunja maduka ya wafanyabiashara ndipo raia wema walipotoa taarifa kwa Jeshi la Polisi.
Askari Polisi waliokuwa doria baada ya kupata taarifa hizo walifika katika eneo la tukio na majambazi walipogundua uwepo wa askari katika eneo hilo walianza majibizano ya risasi ili kujihami.
Advera Bulimba ni Kaimu Kamanda wa polisi Mkoa wa Mwanza amethibitisha kuuawa kwa majambazi hao pamoja na kutoa wito kwa wananchi wanaofanya uhalifu mkoani humo kutojihusisha na matukio ya kihalifu.
Miili ya majambazi hao watatu imehifadhiwa katika hospitali ya Rufaa ya Mwanza Sekoutoure kwa ajili ya utambuzi.








