Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Wanawake hawaelewi rushwa ya ngono"- Mbunge Ayoub

Alhamisi , 24th Mei , 2018

Mwakilishi wa Jimbo la Paje, Jaku Hashim Ayoub ameitaka serikali kuchukua hatua za kuwadhibiti waajiri wanaojihusisha na vitendo vya kuwaomba wanawake rushwa ya ngono kwenye ajira.

Mwakilishi huyo ameyasema hayo katika kikao cha Baraza la Wawakilishi wakati akiuliza swali lake la msingi kuhusu wanawake kudaiwa rushwa ya ngono na wanatakiwa wafanye nini wanapokutana na kadhia hiyo.

Akijibu swali la hilo, Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto, Shadia Mohammed amesema serikali haina takwimu za matukio hayo kwa kuwa wanawake wengi hawaelewi rushwa ya ngono ila viashira huwa vinaonekana na hushindwa kuripoti vitendo hivyo.

"Wanawake wanashindwa kuripoti matukio hayo kwa kuwa wanahofia kuachishwa kazi au kukosa kazi, kwa kawaida rushwa ya ngono hufanyika kwa siri sana tofauti na rushwa nyingine na hufanywa kwa lengo la kupandishwa cheo, mshahara au msaada wowote katika kazi", amesema Shadia.

Aidha, Shadia amesema serikali inaendelea kutoa elimu ya rushwa ili kujenga uelewa wa dhana na maana halisi ya rushwa na kuepukana na matendo hayo.

Kwa upande mwingine, Naibu Waziri huyo amewataka wanawake wanaokumbana na kadhia hiyo kuenda kuripoti Polisi pamoja na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa Zanzibar ili kudhibiti matukio hayo.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa