
Amesema si jambo la heri kumtusi kiongozi mkuu wa nchi kutokana na masuala ya kitaifa hata kama kuna utofauti wa itikadi za vyama.
Akizungumza na wandishi wa habari mshauri huyo wa Mufti amesema ili kiongozi uheshimiwe ni lazima kwanza ujenge misingi ya wewe mwenyewe kuheshimu wengine akiwataka watanzania kuacha mihemko kutusi watawala na kuwadhalilisha.
Akihitimisha katika moja ya mapendekezo amesema ni vyema sasa wenye nia ya kupinga mkataba huo wakasema ni maeneo yapi yarekebishwe kwa kuwa tayari Bunge la Tanzania limepitisha azimio la uwepo wa ushirikiano huo wa awali kati ya Tanzania na Serikali ya Dubai.