Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanafunzi 11 mbaroni kwa tuhuma za kuchoma moto

Jumanne , 20th Jul , 2021

Jeshi la Polisi mkoa wa Geita linawashikilia wanafunzi 11 akiwemo msichana mmoja kwa tuhuma za kuchoma moto shule ya sekondari Geita mara tatu tofauti, Julai 5, 6 na 14 huku likidai chanzo cha kufanya hivyo ni upendeleo waliokuwa wanaupata wanafunzi wanaokaa bweni.

Picha baadhi ya eneo lilioharibiwa na moto katika Shule ya Sekondari Geita (picha kutoka mtandaoni)

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Geita Henry Mwaibambe amesema uchunguzi umeonesha moto ule haukusababishwa na hitilafu ya umeme wala miundombinu chakavu ya shule hiyo, bali umefanywa na wanafunzi watukutu.

“Vinara tunaowashikilia wote ni wanafunzi, baadhi wanafunzi wa shule hii, mmoja ni Frank Joseph maarufu kwa jina la chui, mwengine ni Henry Benedict maarufu kwa jina la panya, hawa ni wanafunzi maarufu na wengine, na mwanamke pekee anaitwa Paskazia Joseph mwanafunzi wa kidato cha tatu, huyu mwanafunzi ana simu, simu ndio anaitumia kupanga mipango amekamatwa na simu na meseji mbalimbali zinazohusiana na uchomaji wa hapa shuleni,” amesema Kamanda Mwaibambe.

Aidha, Kamanda Mwaibambe ameeleza kwamba kutokana na utovu wa nidhamu wa wanafunzi hao wa kutwa shuleni hapo, bodi iliazimia kuondoa wanafunzi wa kutwa ndipo wakapanga njama za uchomaji wa shule hiyo.

“Mpango wa serikali ni ku-phase out wanafunzi wa kutwa kutokana na matatizo ya miaka na miaka ya shule hii ikiwemo kuchomwa fensi, hao waliobakia ambao ni kidato cha 3 na 4 ambao wapo mwishoni kuondolewa ndio wakapanga mpango kwamba tarehe 5 watawakomesha wananfunzi wa bweni,” amesema Kamanda Mwaibambe.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa