
Ahmad Makame, Kamanda wa Polisi mkoa wa Katavi
Inaelezwa kuwa kabla ya tukio hilo la mauaji, wananchi marehemu walimtuhumu kuiba debe mbili za mahindi mali ya Emmanuel Malela, na kiongozi wa mtaa huo aliwaagiza watu wanaomshikilia wamfikishe kituo cha polisi Kanoge ila wakajichukulia sheria mkononi.
Watu hao watano wanaotuhimwa kutekeleza mauaji ya Hamisi wanashikiliwa na Jeshi la Polisi na kupitia kitengo cha upelelezi walibainika kukimbilia mkoani Tabora na kurudishwa Katavi kwa ajili ya kujibu mashtaka yanayowakabili.