majeneza yaliyobeba miili ya watoto
Wakiwa msibani hapo Afisa Ustawi wa Jamii wa halmashuri hiyo Shadrack Nundu, ameisisitiza jamii kufuata ushauri wa wataalamu ili kuepusha vifo visivyotarajiwa huku mkaguzi wa polisi kata ya Nkololo Agnes Henry akiitaka jamii kutokutumia njia za mkato kutatua changamoto zikiwemo za kiafya.
Yohana Saku ni baba mzazi wa watoto hao waliopoteza maisha amesema tayari alikuwa kaanza maandalizi ya kuwapeleka watoto wake shule ili waweze kuendelea na masomo yao badae waje waisaidie familia.
Akiongoza ibada ya mazishi mchungaji wa kanisa la waadventist wasabato ,Chilonge Hezron ameiomba jamii kuachana na imani za kishirikiana na badala yake iwe na hofu ya MUNGU hatua itakayopelekea jamii kuishi kwa kufuata ushauri ulio bora.
Watoto hao walifariki Oktoba 4,2023 na na mara baada ya mazishi yao taratibu za kiserikali zikiendelea.