Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wafanyabiashara 2500 kushiriki sabasaba

Jumatano , 28th Jun , 2017

Washiriki zaidi ya 2500 kutoka ndani na nje ya Afrika wamethibitisha kushiriki Maonesho ya 41 ya biashara ya Kimataifa maarufu kama Sabasaba Julai 1 mwaka huu  yanayotarajiwa kufunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.John Magufuli.

Rais John Pombe Magufuli

Taarifa iliyotolewa na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, amesema Rais Magufuli atafanya ufunguzi huo katika Uwanja wa Maonesho wa Mwalimu Julius Nyerere uliopo barabara ya Kilwa Jijini Dar es Slaam.

Aidha, Waziri Mwijage amesema lengo la maonesho hayo ni kutoa fursa kwa wafanyabiashara wa ndani kujifunza mambo ya biashara na uzalishaji bora wa bidhaa kulingana na soko la kimataifa, kutengeneza mitandao ya mawasiliano baina yao ambayo itawasaidia kukuza biashara na kufikia malengo waliyojiwekeka, kutoa fursa ya kuuza bidhaa zao pamoja na kuruhusu taasisi  mbalimbali kutangaza biashara na huduma bila ya kuwasahu wafanyabiashara wa nje pia.

Picha kutoka Maktaba ikiwa inamuonesha Waziri Mwijage alipokuwa ametembelea banda la wanyama TANAPA

“Maonesho haya yanabeba kauli mbiu isemayo ukuzaji wa biashara kwa maendeleo ya viwanda, inalenga kutumia maonesho haya kama jukwaa la kutangaza biashara na huduma mbalimbali kwa ajili ya ukuzaji wa sekta ya viwanda, ikizingatiwa kuwa serikali ya awamu ya tano inaweka mkazo mkubwa katika kuendeleza uchumi wa viwanda hapa nchini” ilisema taarifa ya Waziri.

Pamoja na hayo, Mwijage amesema maonesho ya mwaka huu yatatoa fursa kwa wenye viwanda vidogo, vya kati na vikubwa kukutana na wanunuzi wa bidhaa zao pamoja na kuwepo na kampeni ya kuhamasisha wananchi kupenda kutumia bidhaa zilizozalishwa hapa nchini.

Mpaka sasa baadhi ya nchi ambazo zitakazoshiriki katika maonesho hayo ni pamoja na Burundi, China, Comoro, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Misri, Ujerumani, Ghana, India, Indonesia, Iran, Italia, Japan, Kenya, Malawi na Mauritius.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa