Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Vyama viwe kichocheo cha maendeleo"- Shibuda

Ijumaa , 25th Sep , 2020

Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini John Shibuda amewataka wagombea wote kutoka vyama mbalimbali kuepuka kupandikiza chuki katika taifa ambapo ameviasa pia vyombo vya dola kusimama imara katika ulinzi wa tunu za Watanzania wakizingatia weledi.

Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini John Shibuda.

Bw. Shibuda ambaye naye pia ni mgombea urais kupitia ADA-TADEA amsema kwamba mfumo wa vyama vingi nchini ni kichocheo cha maendeleo na si kuchochea mafarakano hivyo wagombea wa nafasi mbalimbali kutoka vyama mbalimbali vya siasa katika uchaguzi wa Oktoba 28 wazingatie weledi endapo watapatiwa ridhaa ya uongozi.

"Watanzania tukukumbe Tanzania hii itajengwa na sisi wenyewe tusisahau kuwa maumivu ya leo ni uimara wa kesho Viongozi watakaopata ridhaa ni muhimu kuzingatia utaifa kwanza", amesema John Shibuda.

Katika kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi amevitaka vyama vya siasa vijenge hoja na nasaha kwa Watanzania na kwamba uongo wa siasa huzaa dhuluma kwa vizazi ambavyo havitashiriki kupiga kura kwa kuwa ukweli huzaa haki.

Amesisitiza kuwa siasa ni kaa la moto ukilikanyaga bila kiatu lazima utaungua huku  akivitaka vyama vya Siasa 19, vilivyopata ridhaa kuwania nafasi ya Ubunge na Udiwani pamoja na vyama 15 vilivyopata ridhaa za wagombea wao kuwania nafasi ya Rais kutangaza sera zao kwa Watanzania ili wafanye maamuzi sahihi ifikapo siku ya kupiga kura Oktoba 28, 2020.

HABARI ZAIDI

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani