_0.jpg?itok=g8JGJczI×tamp=1473164275)
Mwanasiasa Mkongwe hapa nchini, Mzee Kingunge Ngombale Mwiru akizungumza na Waandishi wa Habari
Maamuzi hayo yamekuja baada ya baraza kuu kujadili na kutathimini mwenendo wa kamanda huyo hasa kipindi hichi cha mapambano.
Sadifa amesema kuwa wamedhamiria kufanya hivyo baada ya kubaini Kigunge anaonekana kuwa na mapenzi zaidi ya watu kuliko chama hivyo ni bora waachane na mzee huyo ili wazidi kusonga mbele.
Kikao hicho cha baraza kimefikia maamuzi hayo baada ya kuamini kuwa kamanda huyo kwa sasa hataweza kuivusha jumuiya hiyo katika kupata ushindi wa kishindo Oktoba 2015.