
Katibu Mkuu wa UVCCM Fakii Raphael Lulandala
Ameyasema hayo wakati anahutubia wananchi mkoani Dodoma mara baada ya mapokezi yake yaliyofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya UVCCM Dodoma leo Oktoba 4, 2023.
"Kutakuwa hakuna sababu ya kuwa na Katibu wa UVCCM kwenye wilaya zetu, kata zetu na mikoa kama Chama cha Mapinduzi kinashambuliwa katika maeneo yao, ukiona mchungaji wa kondoo amepigwa lengo sio mchungaji ni kondoo" amesema Lulandala.
Aidha amesema katika kupambana na hoja za wapotoshaji na walaghai ni ajenda ya kudumu ya UVCCM.