Jumanne , 17th Sep , 2024

Umoja wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania, umepinga maandamano yanayotaka kufanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Ifikapo Septemba 23, 2024 kwani kufanya hivyo kutaharibu ajenda ya nchi kueleka Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Abdul Mluya, Mwenyekiti Umoja wa Vyama vya Siasa.

Wakiongea kwa niaba ya vyama 13 vya Siasa Mwenyekiti wa umoja huo Abdul Mluya anasema kufanya hivyo kutaharibu mwelekeo wa Serikali kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kuvuruga amani ya nchi.