
Taswira ya Sanamu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere iliyowekwa kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Afrika (AU), Addis Ababa
Kauli hiyo ameitoa hii leo Februari 22, 2024, wakati akizungumza mbele ya wahariri na waandishi wa habari Ikulu ya Dar es Salaam, baada ya kuibuka kwa maoni mchanganyiko kutoka kwa Watanzania ambao wengi wao walisema sanamu hiyo haifanani na Baba wa Taifa, ambapo serikali pamoja na familia ilijiridhisha kuhusu taswira ya sanamu hiyo.
"Kamati ya kutengeneza sanamu ilihusisha wataalam kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ilihusisha familia ya Mwalimu Nyerere akiwemo Madaraka Nyerere ilihusisha watu kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, watu kutoka Wizara ya Utamaduni ambao waliunda jopo la wataalamu na watu wengine wa masuala ya kutengeneza sanamu, kamati iliridhika kwa sababu mwalimu mnayemuona katika sanamu lile la Addis ni mwalimu anayeeelezwa wa miaka ya 60 hadi 80 wakati yuko active katika mapambano ya kusaidia kuleta uhuru na maendelea Kusini mwa SADC," amesema Balozi Shaibu
Aidha ameongeza kuwa "Lakini pia kauli ya mwanae Madaraka Nyerere ameitoa mara kadhaa na mpaka siku ya uzinduzi mimi nilikuwepo Madaraka aliendelea kusisitizxa kwamba yule ni Baba yake na akama kuna mtu ambaye anabisha basi amuulize yeye,".