Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tanzania yaziunganisha benki mbili kuwa moja

Jumatano , 16th Mei , 2018

Benki Kuu ya Tanzania BoT, imeridhia uamuzi wa kuiunganisha Benki ya Twiga Bancorp Ltd na ile ya Tanzania Postal Bank Public limited Company (TPB Plc), ili iwe benki moja yenye nguvu ambayo utendaji wake utakuwa chini ya usimamizi na uendeshaji wa TPB Plc, uamuzi ambao utaanza Mei 17, 2018

Hayo yamebainishwa na Naibu Gavana wa Benki Kuu Dkt. Bernard Kibese wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam leo Mei 16, 2018 na kusema benki hiyo ya Twiga Bancorp iliyokuwa chini ya usimamizi wa benki kuu kwa takribani ya miaka miwili, ambapo mali za wateja na madeni ya benki hiyo kwa sasa yatasimamiwa na benki ya Tanzania Postal Bank Public Limited Company.

Dkt. Kabesema amesema uamuzi huu umechukuliwa ili kuboresha uangalizi na utendaji wa benki zinazomilikiwa na serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuuhakikishia umma kuwa itaendelea kulinda maslahi ya wenye amana katika mabenki kwa lengo la kuleta ustahimilivu katika sekta ya fedha.

Pamoja na hayo, Naibu Gavana Kibese amesema hatua kama hiyo itachukuliwa pia kwa benki nyingine za serikali ambazo ufanisi wake hautokuwa wa kuridhisha, kwani nia ya serikali ni kuwa na benki moja kama sio chache zinazofanya vizuri, malengo ambayo Rais Dkt John Pombe Magufuli amekuwa akisisitiza mara kwa mara.

Kwa upande wake Meneja Uendeshaji wa Bodi ya Bima ya Amana, Bi Rosemery Tenga amewataka walikuwa wateja katika benki ambazo zipo chini ya BOT kufuata mitaji ya benki hiyo kuyumba kwenda katika benki hizo na utaratibu wa malipo utafanyika chini ya usimamizi wa bodi ya Amana.

Uamuzi huo wa BoT umetokana na benki ya Twiga kuwa na upungufu mkubwa wa mtaji ambapo ni kinyume na matwaka ya sheria ya mabenki na taasisi za fedha ya mwaka 2006 na kanuni zake ambapo kwa wakati huo ilihatarisha usalama wa sekta ya fedha.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa