Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Spika Ndugai amenisikitisha- Godbless Lema

Jumatano , 13th Sep , 2017

Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amefunguka na kudai amesikitishwa na kitendo cha Spika wa Bunge, Job Ndugai kuwataka wabunge wawili kufika mbele ya Kamati ya Maadili na mwengine kamati ya ulinzi na usalama kuhojiwa juu ya kauli zao walizozitoa

Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.

Mhe. Godbless Lema amesema hayo leo akiwa mjini Nairobi nchini Kenya alipokwenda kumjulia hali Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu ambaye ameshambuliwa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana. 

"Nimesikitishwa sana na kitendo cha Mhe. Spika kuwataka wabunge wawili, Mhe. Zitto Kabwe na Saed Kubenea kutokea  katika kamati ya maadili na mwingine kamati ya ulinzi na usalama na pengine baada ya maneno yangu haya na mimi naweza nikaitwa lakini siyo kitisho tena kwangu kuitwa mahali popote. Nipo Nairobi kumuangalia mbunge wetu na rafiki yangu, Mhe. Lissu ambaye hawezi kula wala kuinua mkono baada ya kupigwa na risasi na watu wasiojulikana", amesema Lema.

Pamoja na hayo, Lema ameendelea kwa kusema "Nilitarajia Mhe. Spika aliposikia taarifa za mbunge wake kupigwa risasi pengine shughuli za Bunge zote angesimamisha kama ambavyo alivyoamuru kukamatwa kwa wabunge wawili wapelekwe Polisi akiwemo Kubenea hapo awali", amesisitiza Lema.

Spika wa Bunge, Job Ndugai  

Kwa upande mwingine, Mhe. Godbless Lema amedai alitarajia kuona mabadiliko ya katika Bunge kwa kupitisha sheria kwa pamoja ili kusudi wabunge waweze kupatiwa ulinzi wa kutosha kuanzia majumbani kwao mpaka wao wenyewe lakini imekuwa tofauti na yeye alivyokuwa akifikiri.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea