Jumatatu , 22nd Jan , 2024

Zaidi ya wanafunzi 900 wa shule ya msingi Michael Urio uliyopo Kunduchi jijini Dar es salaam wamelazimika kutoendelea na masomo kutokana na shule hiyo kujaa maji kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha

Akizungumza na waandishi wa habari Diwani wa kata ya Kunduchi Michael Urio amesema mpaka sasa wamelazimika kufunga shule hiyo ya Watoto ya mchepuo wa kiingereza kutoendelea na masomo kwa wanafunzi kwa sababu za kiusalama ambapo ameiomba TANROADS kusaidia kujenga mitaro itakayosaidia kutoa maji katika maeneo hayo
Urio amesema kama ambavyo miradi mwingine inapewa kipaumbele kama vile barabara na madaraja basi swala la elimu pia lipewe kiupaumbele

Shule ya Msingi Michael Michael Urio ina wanafaunzi zaidi ya mia nane ambapo kwa mwaka huu zaidi ya wanafunzi 500 wameandikishwa ambapo zaidi ya wanafunzi 900 watakosa kwa kuwa shule hiyo itafungwa mpaka mazingira yatakapokuwa Salama