
Nemes Tarimo
Waziri amesema taarifa walizozipokea ni kwamba mwezi Machi 2022 Mtanzania huyo alikuhumiwa kifungo cha miaka saba gerezani kwa mujibu wa sheria za Urusi kwa vitendo vya uhalifu
Na kwamba akiwa gerezani alipewa nafasi ya kujiunga na kikundi cha kijeshi kilichopo nchini humo kinachofahamika kama Wagner kwa ahadi ya kulipwa fedha lakini pia kwa ahadi ya kuachiwa huru mara baada ya vita na alikubali kujiunga na kikundi hicho
Hata hivyo Waziri Dkt. Tax ameeleza kuwa mwili wa marehemu unawasili leo ingawaje serikali haitahusika na masuala yoyote ya mazishi yake.