![](http://eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2021/07/28/NDUGULILE 11.jpg?itok=Z6sgiMas×tamp=1627483714)
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dk. Faustine Ndugulile
Dk. Ndugulile ameyasema hayo leo Jijini Dodoma ambapo amebainisha kuwa kwa kipindi cha robo mwaka yaani kuanzia Aprili hadi Juni laini elfu 18, 622 zimefungiwa kutokana na kufanya vitendo vya kihalifu kwa njia ya mtandao.
Dk. Ndugulile ameongeza kwa kusema kuwa vitambulisho vilivyotumika kusajilia laini elfu 14,768 vimezuiliwa baada ya kuonekana vinatumika na matapeli na hatua inayofuatia ni kuwafungulia mashtaka Mahakamani wahusika ili kukabiliana na wimbi la utapeli wa mtandaoni.