Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

RC Kilimanjaro alia na TANESCO 'Toeni taarifa'

Jumatatu , 25th Jan , 2021

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira, amelitaka Shirika la umeme nchini (TANESCO), kuhakikisha wanatoa taarifa mapema kabla hawajakata umeme ili isiweze kuleta madhara kwa wananchi na wafanyabishara wakubwa.

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Januari 25, 2021, wakati akizungumza kwenye kipindi cha SupaBreakfast cha East Africa Radio, ambapo amesimulia ni kwa jinsi gani mteja aliyekuwa analipa milioni 100 kila mwezi kama bili ya umeme, alivyoharibikiwa na mtambo wake wa kutengeneza nondo baada ya umeme kukatika.

"Nina mfanyabiashara ambaye anazalisha chuma alikuwa keshafika mbali sana, siku moja amechoma chuma chake cha kutengeneza nondo na amenunua kinu cha fedha nyingi, chuma kile kimeshayeyuka anataka sasa aanze kutengeneza nondo umeme ukakatika,  kile chuma kikawa jiwe, kinu kikafa, kipindi hicho alikuwa analipa bili ya umeme ya milioni 100 kila mwezi", amesema RC Mghwira

Aidha RC Mghwira ameongeza kuwa, "Hata kama tunazalisha umeme kidogo, TANESCO watupe taarifa, mfano mimi Meneja akinitumia message ya hitilafu na ikifika tu nawasambazia wananchi wangu, wakuu wa wilaya na wenyewe nawaambia sambazeni, nina orodha ya wazalishaji wetu wakubwa wote nawaambia jamani kutakuwa na hitilafu ya umeme"
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa