Ijumaa , 8th Jul , 2022

Waziri Wa Afya Ummy Mwalimu, amesema serikali inafanya mapitio ya polyclinic zote nchini ili kubaini vigezo vyake kwa sababu zimekuwa kichochoro cha udanganyifu.

Waziri Wa Afya, Ummy Mwalimu.

Waziri Ummy, amesema hayo leo Julai 8, 2022, wakati wa mkutano wake na watoa huduma za afya wa umma na binafsi kwa mkoa wa Dar es Salaam.

Katika hatua nyingine Waziri Ummy, amesema hadi kufikia mwezi Desemba mwaka huu itakuwa imekamilisha mpango wa bima ya afya Kwa wote ambao utakuwa ni lazima.