Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Nimejaribu kuwasiliana naye sijampata" - Mdhamini

Jumatatu , 14th Sep , 2020

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, leo Septemba 14, 2020, imeahirisha kesi inayowakabili Tundu Lissu na wenzake ya kuandika habari za uchochezi kinyume na sheria ya magazeti ya mwaka 2002, baada ya washitakiwa wawili kushindwa kufika mahakamani.

Tundu Lissu.

Washtakiwa ambao hawakufika mahakamani hapo ni pamoja na mgombea Urais kupitia CHADEMA Tundu Lissu na Ismail Mehboob.

Akizungumza mahakamani hapo mdhamini wa Tundu Lissu ,Robert Katula amedai kuwa amejitahidi kumtafuta mshitakiwa huyo lakini hakumpata.

"Nimejaribu kuwasiliana nae sijampata mpaka sasa hivi, nimeongea na rafiki zake wamesema amebanwa na ratiba ya Tume ya Uchaguzi hivyo tunaomba Mahakama ipange tarehe nyingine", amesema Katula

Kwa upande wake Wakili Mwandamizi wa Serikali, Wankyo Simon wakati akizungumza mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Thomas Simba, amesema kuwa shauri hilo lilifikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa na kuomba ipangwe tarehe nyingine.

Ambapo Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 15, 2020, itakapotajwa tena ambapo washtakiwa wote wapo nje kwa dhamana.

Katika kesi ya msingi Lissu na wenzake wanakabiliwa na mashtaka matano likiwemo la kupanga njama za kuchapisha taarifa za uchochezi.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa