
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwenye tume hiyo ya uchaguzi (INEC) imesema kwamba vyama vya siasa 18 viliwateua wagombea wake na manaibu wagombea Urais.
Moja ya majina makubwa yaliyomo ni lile la mwanasiasa mkongwe nchini humo mwenye umri wa miaka 75 ambaye ni makamu wa zamani wa Rais nchini humo Atiku Abubakar kutoka chama pinzani cha Peoples' Democratic Party, akiwemo pia gavana wa zamani wa jiji la Lagos Bw.Ahmed Bola Tinubu,mwenye umri wa miaka 70 wa chama tawala cha cha All Progressives Congress.
Ukosefu mkubwa wa usalama, ukosefu wa ajira na uchumi mbaya vinatarajiwa kuwa ajenda kubwa kwenye uchaguzi huo ujao. Nigeria ina watu zaidi ya milioni 200 ambapo watu milioni 95 wameshajiandikisha kupiga kura nchini humo.
Kampeni za uchaguzi zinatarajiwa kuanza kuridnima jumatano wiki ijayo