Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

NEMC yaonya wanaoingiza vibebeo vilivyokatazwa

Ijumaa , 11th Sep , 2020

Serikali imetoa onyo kwa wafanyabiashara nchini ambao bado wanaendelea kuingiza vibebeo vilivyopigwa marufuku kwa mujibu wa kanuni ya sheria za mazingira na kuwataka wafanyabiashara kuendelea kubadilisha fikra kwa kuwa Mpango uliopo ni kuondoa kabisa malighafi zote zenye madhara.

Mkurugenzi Mkuu (NEMC)Dk Samuel Gwamaka katika mahojiano na EATV ofisini kwake

Onyo hilo  limetolewa na Mkurugenzi Mkuu kutoka Baraza la Taifa la hifadhi na usimamizi wa Mazingira (NEMC)Dk Samuel Gwamaka kufuatia kuwepo kwa wafanyabiashara wachache wenye vitendo hivyo akibainisha kuwa kitu chochote cha kisichooza ni hatari kwenye mazingira.

"Tumekuwa tukitoa maonyo kila Mara lakini bado kuna wafanyabiashara wasio waaminifu wanatumia njia za panya kuingiza vibebeo vilivyopigwa marufuku na serikali kwa sasa tukikukamata tutakufungulia mashitaka na ukibainika kwa mujibu wa Sheria za nchi wachukuliwe hatua kali "-Dk Samuel Gwamaka.

Katika mahojiano na EATV  amezitaka halimashauri zote nchini kuhakikisha wanaweka  utaratibu wa kufanya utafiti juu ya aina za taka zinazozalishwa katika maeneo mbalimbali ili iwe  rahisi kuzisafirisha kwenda mahali husika.

"Nitumie fursa hii kutoa ushauri kuwa manispaa zote kufanya tafiti juu ya taka zinazozalishwa kwenye maeneo yao kwa kuwa nyingi hazikusanywi inavyostahili kutokana na changamoto mbali mbali baraza lipo na wataalamu wako hapa tuko tayari kuwaelekeza mbinu rahisi zenye gharama nafuu katika kuyalinda mazingira yetu"alisema Dk Gwamaka Mkurugenzi Mkuu NEMC.

Takataka zimetajwa kuwa fursa ambayo jamii inaweza kuitumia kwa kuzikusanya kwa aina ya makundi yake na kuzirejeleza hali inayoweza kuongeza kipato kwa mtu na taifa  kutokana na uwekezaji wa viwanda.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa