
Mohammed Bin Saleh Al-Sada - Rais wa OPEC
Rais wa OPEC Mohammed Bin Saleh Al-Sada, amesema punguzo la mapipa milioni 1.2 kwa siku litaanza kuanzia mwezi Januari mwakani hatua ambayo inafuatia kushuka kwa bei ya mafuta kulikodumu kwa miaka miwili.
Kufuatia hatua hiyo ya OPEC ya kupunguza uzalishaji wa mafuta, nchi zinazozalisha mafuta ambazo siyo mwanachama wa OPEC nazo zinatarajiwa kupunguza uzalishaji kwa mapipa 600,000 kwa siku kulingana na taarifa iliyotolewa na Rais wa Opec Al-Sada.