Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

NAOT watoa msaada kwa watoto yatima Dodoma

Jumamosi , 25th Jun , 2022

Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) wamekabidhi msaada kwa kituo cha watoto yatima kilichopo Kijiji cha Matumaini jijini Dodoma. Msaada huo umekabidhiwa kwa mlezi wa Kituo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo huadhimishwa mwezi Juni kila mwaka.

Akizungumza kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Naibu Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali – Divisheni Serikali za Mitaa, Bw. Benjamin Mashauri amesema utoaji wa msaada huo ni sehemu ya hatua mbalimbali zilizopendekezwa katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2022.

“Kwa namna ya pekee naomba upokee salamu za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, ambae anatambua kazi kubwa mnayoifanya katika kituo hiki ya kulea watoto na Ofisi yetu itaendelea kutoa misaada kwa jamii kadri itakavyowezekana,” amefafanua zaidi Mashauri. Msaada uliotolewa kwa kituo ni pamoja na mchele, sukari, maji ya kunywa, maziwa ya unga aina ya lacktojeni kwa watoto wachanga, sabuni za kufulia, sabuni za kuogea, mafuta ya kupikia, soda, juisi na zawadi nyingine za kuwapa watoto faraja.

Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ni moja ya matukio muhimu katika kalenda ya Umoja wa Afrika (AU) ambapo nchi wanachama huadhimisha kwa kufanya maonyesho ya kazi mbalimbali na Kongamano kuhusu masuala ya Utumishi wa Umma. Moja kati ya shughuli zilizotekelezwa katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka huu ilikuwa ni pamoja na kufanya shughuli za kijamii ili kujenga mahusiano mazuri na Wananchi.


Kwa kutambua kwamba Kijiji cha Matumaini kinatoa mchango mkubwa katika kuunga mkono juhudi za Serikali za kuboresha ustawi wa jamii hususani katika kulea na kutunza watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu. Mbali na kukabidhi msaada huo wa Ofisi, Wafanyakazi walioshiriki kwenye tukio hilo waliendesha harambee fupi na kukusanya zaidi ya Shilingi Milioni 1 na laki 4 ambazo walizikabidhi kwa Kituo ili ziweze kusaidia mahitaji ya Kituo.

HABARI ZAIDI

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani