Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Naomi atupwa jela miezi minne kisa gongo

Jumatano , 24th Mei , 2023

Naomi Jeremiah (25), mkazi wa Kata ya Mabatini wilayani Nyamagana jijini Mwanza, amehukumiwa kifungo cha miezi minne gerezani au kulipa faini ya shilingi laki nne kwa kosa la kukutwa na lita 125 za pombe ya moshi maarufu kama gongo.

Naomi Jeremiah

Hukumu hiyo imetolewa katika Mahakama ya Mwanzo Nyamagana na Hakimu Mariam Omary baada ya kumtia hatiani mshtakiwa huyo kwa mujibu wa kifungu cha 32 cha kanuni ya mwenendo wa mashauri ya jinai ya mahakama za mwanzo jedwali la tatu, sheria ya mahakama na mahakimu sura ya 11 mapitio ya mwaka 2019.

Imeelezwa kuwa mnamo tarehe 11 ya mwezi huu Askari Polisi wakiwa kwenye doria eneo la mabatini walimkamata nyumbani kwake Naomi Jeremiah akiwa na pombe hiyo ya moshi lita 125 kisha kumpeleka kituo cha polisi na kumfungulia kesi namba 1239 ya kupatikana na pombe hiyo haramu.

Akitoa Ushahidi wake katika Mahakama ya Mwanzo Nyamagana Kaimu Mkuu wa Upelelezi wilaya ya Nyamagana aitwaye Makia Katani, aliyeongoza msako dhidi ya uhalifu na wahalifu ameiambia mahakama hiyo kuwa taarifa ya mshtakiwa kuhusika na biashara ya pombe hiyo haramu waliipata kutoka kwa wananchi ndipo wakaenda kukagua na kukamata lita 125 za pombe hiyo ya moshi.

Mara baada ya kufikishwa mahakamani mshtakiwa huyo alikiri kutenda kosa hilo ambapo mahakama ikamtia hatiani kwa mujibu wa kifungu cha 30 sheria namba 62 ya mwaka 1966, na kumfunga kifungo cha miezi minne gerezani au kulipa faini ya shilingi laki nne na kuamuru pombe hiyo kuharibiwa kwa kumwagwa.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa