Ikiwa hii ni wiki ya sheria yenye kauli mbio inayosema, umuhimu wa utatuzi wa migogoro kwa njia ya usulushi wajibu wa mahakama na wadau, kwa Mkoa Mtwara uzindua umefanyika katika Mahakama kuu kanda ya Mtwara, ambapo inabainika kuwapo kwa kesi chache katika mahakama ya Mwanzo Msimbati, baada ya kugundua uwapo kwa Mzee Issa Mkumba, ambaye amekuwa akitatua migogoro kwa wakazi wa eneo hilo,
Jaji Mfawidhi Mahakama kuu Kanda ya Mtwara Zainabu Muruke, ametoa rai kwa wakazi wa Mkoa wa Mtwara, kutatua migogoro yao kwa njia ya usuluhishi, badala ya kukimbilia mahakamani ambapo wamekuwa wakipoteza muda mwingi, na kushindwa kufanya kazi za kujiingizia kipato.