Waziri wa TAMISEMI Ummy Mwalimu
Kauli hiyo ameitoa hii leo Januri 6, 2021, wakati akitoa tamkoa maalum kwa wanafunzi wanaotarajiwa kuanza masomo Januari 17, huku akimshukuru Rais Samia kwa kuwezesha ukamilikaji wa madarasa 12,000 nchini.
"Kama ni mwanafunzi wa sekondari anaweza akatumia sare yake aliyokuwa anavaa shule ya msingi wakati mzazi anatafuta fedha au akavaa tu t-shirt na sketi yake nzuri akaenda darasani, wazazi pia waangalie joining instruction (maelekezo ya kujiunga na shule) inasema nini kwa sababu kuna vitu vingi ambavyo havina hata umuhimu, jamani tuondoe vikwazo," amesema Waziri Ummy.